99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Wataalamu waitaka EAC kukubali Kiswahili kuwa lugha rasmi ya kikanda

(CRI Online) Julai 09, 2024

Wataalamu wamerejea tena mwito kwa baraza la mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kuharakisha marekebisho ya Mkataba wa EAC kuiwezesha lugha ya Kiswahili kuwa lugha rasmi ya kanda hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na makao makuu ya Jumuiya ya EAC huko Arusha, wataalamu hao wamezitaka nchi zote wanachama kutunga sheria ya kuhimiza matumizi ya Kiswahili katika shughuli iliyofanyika huko Mombasa.

Waziri wa jinsia, utamaduni, sanaa na urithi wa Kenya Bi. Aisha Jumwa amesema, Kiswahili ni lugha ya umoja katika kanda hiyo, inayotumiwa na watu zaidi ya milioni 200. Amehimiza nchi zote wanachama wa EAC kuhimiza sheria na sera ziandikwe na kuchapishwa kwa lugha ya Kiswahili.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha