99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Wataalamu wakutana nchini Kenya kujadili sera za kodi barani Afrika

(CRI Online) Mei 30, 2024

Wataalamu wanakutana Nairobi, Kenya kuanzia siku ya Jumatano kujadili mikakati ya kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani kupitia hatua madhubuti za kodi barani Afrika.

Mkutano huo wa 9 wa Kodi Afrika wa mwaka 2024 ambao utafanyika kwa siku tatu umeleta pamoja ujumbe wa watu zaidi ya 200, wakiwemo wasimamizi wa kodi wa Afrika na washirika wa maendeleo, kushughulikia masuala muhimu ya kodi kama vile mapato kutokana na biashara za kuvuka mipaka.

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato ya Kenya, Humphrey Wattanga Mulongo, ametoa wito kwa nchi za Afrika kufanya usimamizi wa kodi na ukusanyaji wa mapato kuwa wa kisasa licha ya kukabiliwa na changamoto kama vile uzembe, ukosefu wa uongozi mzuri na mtiririko haramu wa fedha.

Pia ametoa wito kwa wasimamizi wa kodi wa Afrika kulinda haki za walipa kodi, kuzingatia uadilifu, haki, na uwajibikaji wakati wa kuhudumia wateja, na kufanya mifumo madhubuti ya utatuzi wa migogoro kufikiwa kwa urahisi.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha