99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Tanzania yashinda Mashindano ya TEHAMA China

(CRI Online) Mei 29, 2024

Vijana watatu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM) nchini Tanzania Ndaki ya Teknolojia za Habari na Mawasiliano (TEHAMA), wameibuka washindi katika mashindano ya TEHAMA duniani ya Huawei yaliyofanyika kuanzia tarehe 23 hadi 26 mwezi huu huko Shenzhen, China.

Vijana hao Dickson Mram, Matimu Mahimbo na James Amos ambao wana ujuzi katika uhandisi wa kompyuta, TEHAMA na mawasiliano ya simu, walishiriki katika mashindano hayo yaliyoshindanisha wanafunzi zaidi ya 470 kutoka nchi 49 duniani.

Kufuatia ushindi huo, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari nchini Tanzania, Nape Nnauye, amewapongeza kwa kueleza kuwa ushindi huo unaonesha uwezo uliopo miongoni mwa vijana wa Tanzania katika fani muhimu za Teknolojia ya Habari na Mawasiliano.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha