99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Wataalamu wakutana Kenya kujadili njia za kukabiliana na dharura za ukame katika Afrika Mashariki

(CRI Online) Mei 29, 2024

Wataalamu wameanza mkutano wao siku ya Jumanne huko Nairobi nchini Kenya ili kujadili njia za kukabiliana na dharura za ukame katika eneo la Afrika Mashariki.

Mkutano huo wa siku mbili unahudhuriwa na wadau 150 kutoka Mamlaka ya Kiserikali kwa ajili ya Maendeleo ya Nchi za Afrika Mashariki (IGAD), ili kuimarisha ushirikiano katika kuboresha uwezo wa kukabiliana na maafa ya ukame katika ardhi kame na nusu kame.

Naibu Katibu Mtendaji wa IGAD, Mohamed Ware, amesema kuwa watu wa jamii za mpakani, wengi wao ni wafugaji na wakulima, ambao wanategemea mvua zinazoendelea kutokuwa na uhakika. Kutokana na kukosekana kwa miundombinu katika maeneo ya mpakani, juhudi za kibinadamu na misaada mara nyingi inakuwa michache na inachelewa mno kwa waathirika.

Ametoa wito kwa eneo hilo kutekeleza mifumo thabiti ya tahadhari za mapema ili kuboresha uwezo wa kutabiri na kukabiliana na majanga ya ukame.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha